Na Gerald Lwomile
Maonesho ya Vyuo Vikuu nchini yameingia siku ya tatu leo Julai 28, 2021 huku idadi ya wanafunzi wanaotaka kujiunga na masomo ya juu ikiendelea kuongezeka
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na SUA wanafunzi wengi wamejitokeza kuomba nafasi ya kujiunga na masomo katika chuo hicho cha Kilimo na Sayansi zinazoendana na kilimo lakini pia kikawa na kozi mbalimbali ambazo si za sayansi moja kwa moja
Akizungumza katika viwanja vya Mnazi Mmoja ambako maonesho hayo yanaendelea Mratibu wa maonesho hayo SUA Dkt. Innocent Babili amesema wanaridhishwa na idadi ya wanafunzi wanaoomba kujiunga na SUA na kutoa wito kwa wanafunzi wengine kuendelee kuomba huku wao wakisimama kama mshauri katika uchaguzi wa kozi kwa wananafunzi
Habari picha hapa chini
Muonekana wa banda la SUA katika maonesho ya TCU 2021
Watu mbalimbali wamejitokeza kuomba Udahili SUA
Dkt. Babili kulia akizungumza katika mahojiano na mwandishi wa habari Ali Thabiti kutoka Radio Mtwara ambaye pamoja na ulemavu wake wa kutoona lakini alitaka kujua SUA inafanya nini katika maonesho hayo