SUAMEDIA
No Result
View All Result
  • MWANZO
  • HABARI
    • All
    • Kimataifa
    • Kitaifa
    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Human Rights Watch yahimiza uchunguzi wa kuaminika kuhusu miili iliyokutwa mtoni DRC

    Mubashara: Asubuhi hii: Mwili wa Hayati Mkapa kuelekea uwanja wa Uhuru

    LIVE: Mwili wa Rais Mkapa unaagwa Uwanja wa Uhuru, Mkewe aishiwa nguvu, Magufuli, majonzi yatawala

    BOOK OF THE WEEK- “Increasing Production from the Land: A Source Book on Agriculture for Teachers and Students in East Africa” 

    Mubashara:Kinachoendelea msibani kwa Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa muda huu

    Nafasi za Kazi katika Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa

    Tume ya Uchaguzi yabadili majina ya Majimbo matatu, yatangaza Tarehe ya Kutoa Fomu

    Rais Mkapa (Kuzaliwa, Elimu, Uongozi na Urais)

    • Kitaifa
    • Kimataifa
    • MAGAZETI
  • MAKALA
    • All
    • Hifadhi, Utalii na Mazingira
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    BOOK OF THE WEEK- “Increasing Production from the Land: A Source Book on Agriculture for Teachers and Students in East Africa” 

    VIDEO: SUA imeendeleza mkakati wa kuhakikisha wadau wa Elimu wanafikiwa kwa njia ya Elimu Masafa

    Video: Kilimo cha mbogamboga kwa kutumia viroba

    Naibu Waziri wa Ardhi Dkt. Mabula aipongeza Wizara Ya Ardhi kuwezesha Nchi kufikia Uchumi Wa Kati

    Serikali yazindua Chanjo za Kimkakati 13 za Mifugo, Waziri Mpina awaweka kitanzini Wakurugenzi

    Bupilipili: SUA inafanya mambo yake kwa vitendo ikiwa ni pamoja na utalii

    VIDEO: Katavi Mkoa wa Kilimo na Utalii unaotendea haki kasi ya maendeleo ya Serikali ya Awamu ya Tano

    Vyuo vya Kilimo nchini vyatakiwa kujiimarisha kimapato

    • Kilimo
    • Hifadhi, Utalii na Mazingira
    • Ufugaji na Uvuvi
  • TAFITI
  • MICHEZO & BURUDANI
  • 101.1 SUA FM
  • SUA TV
  • SUAMEDIA BLOG
SUBSCRIBE YOUTUBE
  • MWANZO
  • HABARI
    • All
    • Kimataifa
    • Kitaifa
    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Human Rights Watch yahimiza uchunguzi wa kuaminika kuhusu miili iliyokutwa mtoni DRC

    Mubashara: Asubuhi hii: Mwili wa Hayati Mkapa kuelekea uwanja wa Uhuru

    LIVE: Mwili wa Rais Mkapa unaagwa Uwanja wa Uhuru, Mkewe aishiwa nguvu, Magufuli, majonzi yatawala

    BOOK OF THE WEEK- “Increasing Production from the Land: A Source Book on Agriculture for Teachers and Students in East Africa” 

    Mubashara:Kinachoendelea msibani kwa Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa muda huu

    Nafasi za Kazi katika Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa

    Tume ya Uchaguzi yabadili majina ya Majimbo matatu, yatangaza Tarehe ya Kutoa Fomu

    Rais Mkapa (Kuzaliwa, Elimu, Uongozi na Urais)

    • Kitaifa
    • Kimataifa
    • MAGAZETI
  • MAKALA
    • All
    • Hifadhi, Utalii na Mazingira
    • Kilimo
    • Ufugaji na Uvuvi
    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo

    BOOK OF THE WEEK- “Increasing Production from the Land: A Source Book on Agriculture for Teachers and Students in East Africa” 

    VIDEO: SUA imeendeleza mkakati wa kuhakikisha wadau wa Elimu wanafikiwa kwa njia ya Elimu Masafa

    Video: Kilimo cha mbogamboga kwa kutumia viroba

    Naibu Waziri wa Ardhi Dkt. Mabula aipongeza Wizara Ya Ardhi kuwezesha Nchi kufikia Uchumi Wa Kati

    Serikali yazindua Chanjo za Kimkakati 13 za Mifugo, Waziri Mpina awaweka kitanzini Wakurugenzi

    Bupilipili: SUA inafanya mambo yake kwa vitendo ikiwa ni pamoja na utalii

    VIDEO: Katavi Mkoa wa Kilimo na Utalii unaotendea haki kasi ya maendeleo ya Serikali ya Awamu ya Tano

    Vyuo vya Kilimo nchini vyatakiwa kujiimarisha kimapato

    • Kilimo
    • Hifadhi, Utalii na Mazingira
    • Ufugaji na Uvuvi
  • TAFITI
  • MICHEZO & BURUDANI
  • 101.1 SUA FM
  • SUA TV
  • SUAMEDIA BLOG
No Result
View All Result
SUAMEDIA
No Result
View All Result
Home

Virusi vya corona: Trump akubali janga la corona ‘litaathiri vibaya’ kabla ya hali kuimarika

by Tatyana Celestine
July 22, 2020
min read8 min
2

RELATED POSTS

Human Rights Watch yahimiza uchunguzi wa kuaminika kuhusu miili iliyokutwa mtoni DRC

SADC yazipongeza Tanzania na Mauritius kupanda kiuchumi

Nchiza SADC zatakiwa kupambana na Ugaidi na Utakatishaji Fedha Haramu

Buy JNews
ADVERTISEMENT

Rais wa Marekani Donald Trump ameonya kuwa mwenendo wa ugonjwa wa corona nchini humo huenda ukawa “mbaya zaid kabla ya hali kuimarika”, wakati alipofufua tena mkutano wake na wanahabari.

Bw. Trump pia ametoa wito kwa Wamarekani wote kuvalia barakoa, akisema kuwa “zitasaidia kudhibiti maambukizi” na kwamba ni ishara ya “uzalendo”.

Rais, hakua amevalia barakoa wakati akitoa maelezo kwa wanahabari, lakini aliwahi kupuuza suala la kuvaa kifaa kinga hicho.

Inasemekana wasaidizi wake wamemuasa kuchukua hatua zenye malengo wakati ambapo maambukizi yanazidi kuongezeka kote Marekani.

Utoaji taarifa kuhusu corona kwa vyombo vya habari kutoka Ikulu ya Marekani, mwisho ilikuwa Aprili punde tu baada ya Trump kusema kuwa virusi hivyo vinaweza kutibiwa kwa watu kujipaka dawa za kuua vijidudu.

  • Hatimaye Trump avaa barakoa
  • Nani anapaswa kuvaa barakoa kujikinga na corona?

Baada ya miezi kadhaa, taarifa yake ya Jumanne ambayo ilionekana kupangwa, rais aliashiria kuunga mkono kile ambacho maafisa wa afya wamekuwa wakisema kupitia jopo lake la kukabiliana na ugonjwa huo na kuonya kwamba: “Kwa bahati mbaya hali huenda ikawa mbaya zaidi kabla ya kuanza kubadilika.

“Wakati mwingine huenda sipendi kusema kuhusu mambo, lakini hivyo ndivyo ilivyo.”

Aliongeza: “Tunataka kila mmoja ikiwa atashindwa kutekeleza kanuni ya kutokaribiana, avae barakoa.

“Ama uwe unapenda barakoa au la, zina machango wake, zitakuwa na athari yake na tunahitaji kila kitu tunachoweza kupata.”

Bwana Trump – ambaye zaidi ya mara moja alirejelea kuwa ugonjwa wa Covid-19 ni “virusi vya China” – akiwa anatoa taarifa hiyo, alitoa barakoa mfukoni kwake, lakini hakuivaa.

Rais huyo ana kibarua kigumu wakati anapotafuta kuchaguliwa tena kwenye uchaguzi wa urais Novemba dhidi ya mpinzani wake wa chama cha Democratic, Joe Biden, kulingana na kura za maoni.

Bwana Biden Jumanne alimshutumu Bwana Trump kwa kushindwa kukabiliana na janga la virusi vya corona. “Amewaondokea nyinyi, ametenga nchi hii,” aliyekuwa makamu rais wa Marekani alisema.

Coronavirus
  • Coronavirus: Kwa nini ni hatari kugusa uso wako
  • Jinsi ya kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona
  • Majibu ya maswali 10 yanayoulizwa sana kuhusu coronavirus
  • Je unaweza kupata coronavirus mara mbili?
Banner

Kufuata yaliyokuwa yameandikwa tu

Donald Trump ameanza tena kutoka taarifa kuhusu virusi vya corona. Bila kuzingatia alichosema, ukweli tu wa kwamba ameanza tena kutoa taarifa juu ya corona kunaashiria mengi kuhusu athari hasi ya janga hilo ambazo zimekumba Marekani katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Maambukizi yanazidi kuongezeka, hasa kusini na magharibi, hilo pengine moja kwa moja limetokana na hatua ya utawala wake ya kusitisha kanuni za kuzuia usambaaji kabla ya malengo ya wizara ya afya kufikiwa.

Hivyo basi rais alijitahidi sana kuzungumza kulingana na taarifa aliyoandaliwa, na bila kujikanganya akakiri huenda hali ikawa mbaya zaidi kabla ya kuanza kuimarika. Baada ya kipindi kilichotangulia kudai kwamba mwanahabari aliyekuwa amevaa barakoa kuwa yuko sahihi kisiasa”, sasa ahamasisha watu kuvaa barakoa.

President Trump wearing a mask at Walter Reed military hospital, 11 July 2020

CHANZO CHA PICHA,REUTERS

Maelezo ya picha,“Nadhani ni jambo zuri kuvaa barakoa,” rais Trump alisema

Kura za maoni za hivi karibuni zimeonesha kwamba anaendelea kupoteza uungwaji mkono na umma kama rais kuhusu jinsi anavyoshughulikia janga la virusi vya corona wakati anatafuta kuchaguliwa tena.

Ikulu ya Marekani ina imani ya kumwezesha rais kuwa tena chaguo la raia wa Marekani na kufanikisha kurejesha imani ya uongozi wake kwa raia.

Hata hivyo kwa changamoto ya rais sasa hivi kupata ufumbuzi, ni pale tu maambukizi yatakapoanza kupungua, wagonjwa kupungua hospitalini, raia wa Marekani watakaporejea makazini, shule zitakapofunguliwa, na maisha kurejea kidogo kama ilivyokuwa kawaida. Na siku hiyo bado inaonekana kuwa mbali, huku uchaguzi ukikaribia.

line

Bwana Trump alikuwa peke yake bila wataalamu wa afya ambao awali pia nao walikuwa wakitoa taarifa kwa vyombo vya habari. Kauli zake zilikuwa fupi na zenye kuonesha muelekeo, akikwepa kujibizana na wanahabari waliouliza maswali kidogo.

Aliendelea: “Tunawataka Wamarekani wavae barakoa, wazingatie kutokaribiana na kutekeleza usafi wa juu – nawa kimono yako kila unapopata fursa ya kufanya hivyo.

“Tunaomba vijana wa Marekani kuepuka maeneo ya baa yaliyosongamana na mikusanyiko mingine ya ndani. Kuwa salama na mwenye akili.”

Bwana Trump mwenyewe amekuwa havai barakoa mbele ya vyombo vya habari, akidai kwamba baadhi ya watu wanavaa tu barakoa ili kutoa taarifa za kisiasa dhidi yake. Hivi karibuni, vyombo vya habari vilimpiga picha akiwa amevaa barakoa kwa mara ya kwanza wakati alipokuwa anatembelea hospitali ya jeshi.

Alipoulizwa Jumanne kuhusu kubadilika kwake hadi kuanza kuunga mkono uvaaji wa barakoa, rais alisema kwamba hata wataalamu wa afya wamebadili mawazo yao.

Machi, Dkt. Anthony Fauci, mmoja wa viongozi wa jopo la rais la kukabiliana na virusi vya corona, na mpasuaji maarufu Marekani Jerome Adams walisema hakuna sababu ya raia wa Marekani kuvaa barakoa.

Lakini tangu Aprili, Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Marekani (CDC) kimetoa wito kwa raia wa Marekani kuvaa barakoa wanapokuwa maeneo ya umma.

Dkt. Fauci sasa anasema kwamba mamlaka ya Marekani inastahili kutumia nguvu kuhakikisha raia wanavaa barakoa, ingawa Bwana Trump amekataa wito wa Ikulu ya Marekani kutoa agizo la kuvaa barakoa kwa lazima.

Wakati wa mkutano huo, aliendeleza dai la kwamba siku moja ugonjwa huo utatokomea.

Pia alitoa dai la uongo kwamba Marekani ina “idadi ndogo ya vifo vinavyotokana na virusi vya corona, kuliko kwengine kokote duniani”.

Kulingana na chuo kikuu cha Johns Hopkins, idadi ya vifo Marekani inaorodheshwa ya 10 kati ya nchi 20 zilizoathirika vibaya na janga la virusi vya corona duniani.

Marekani imerekodi karibia maambukizi milioni 3.9 ya ugonjwa wa Covid-19 ikiwa na vifo zaidi ya 141,000 miongoni mwa idadi kubwa duniani.

Bwana Trump pia aliulizwa na mwanahabari kuhusu Ghislaine Maxwell, mwenye ushawishi katika mitandao ya kijamii ambaye alihukumiwa mwezi huu na mamlaka ya Marekani kwa makosa ya ulanguzi wa watoto kingono kwa ajili ya aliyekuwa mchumba wake, aliyehukumiwa kwa makosa ya uhalifu wa kingono marehemu Jeffrey Epstein.

Rais alisema: “Sijafuatilia sana kesi hiyo. Ukweli ni kwamba namtakia kila la kheri. Nimekutana naye mara kadhaa, hasa tangu nilipokuwa ninaishi eneo la ufuo la Palm [Florida], na nafikiri pia wao waliishi ufuoni Palm.”

“Sijui hali ya mwanamfalme Andrew,” Bwana Trump aliongeza, akizungumzia Andrew wa familia ya Kifalme Uingereza, ambaye amekanusha madai kuwa alishiriki mapenzi na wasichana wadogo anayesema alisafirishwa na Epstein.

Source: BBC SWAHILI
Via: SUAMEDIA
ShareTweetPin

Tatyana Celestine

Related Posts

Human Rights Watch yahimiza uchunguzi wa kuaminika kuhusu miili iliyokutwa mtoni DRC

August 13, 2020

SADC yazipongeza Tanzania na Mauritius kupanda kiuchumi

July 16, 2020

Nchiza SADC zatakiwa kupambana na Ugaidi na Utakatishaji Fedha Haramu

July 14, 2020

Virusi vya corona: Florida imerekodi idadi kubwa ya maaambukizi ya Covid-19 ndani ya saa 24

July 13, 2020
Kimataifa

SUA kuandaa sera ya kudhibiti udhalilishaji wa kingono

July 8, 2020
Hifadhi, Utalii na Mazingira

Bupilipili: SUA inafanya mambo yake kwa vitendo ikiwa ni pamoja na utalii

July 8, 2020
Next Post

Dirisha la uhamisho EPL kufunguliwa Julai 25

LEO Yanga na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro

Comments 2

  1. Marquis Kwack says:
    2 months ago

    optimal

  2. best car donation charities says:
    2 months ago

    With thanks for sharing your superb website!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published.

HABARI MPYA

  • Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo chapongezwa kwa ubunifu katika Kilimo
  • Habari katika Magazeti ya leo Jumatatu August 17
  • Habari katika Magazeti ya leo Ijumaa August 14
  • Human Rights Watch yahimiza uchunguzi wa kuaminika kuhusu miili iliyokutwa mtoni DRC
  • Mubashara: Asubuhi hii: Mwili wa Hayati Mkapa kuelekea uwanja wa Uhuru
  • MWANZO
  • HABARI
  • MAKALA
  • TAFITI
  • MICHEZO & BURUDANI
  • 101.1 SUA FM
  • SUA TV
  • SUAMEDIA BLOG

© 2020 Sokoine University of Agriculture Media, Tanzania

No Result
View All Result
  • MWANZO
  • HABARI
    • Kitaifa
    • Kimataifa
    • MAGAZETI
  • MAKALA
    • Kilimo
    • Hifadhi, Utalii na Mazingira
    • Ufugaji na Uvuvi
  • TAFITI
  • MICHEZO & BURUDANI
  • 101.1 SUA FM
  • SUA TV
  • SUAMEDIA BLOG

© 2020 Sokoine University of Agriculture Media, Tanzania